logo
swahili
Tumepata Papa mpya
tokea saa limoja
Tumepata Papa mpya

Baada ya mchakato wa siku mbili wa upigaji kura, makadinali 133 wamefanya maamuzi kuhusu Papa mpya atakayeongoza Kanisa Katoliki duniani.

Waumini waliokuwa wakisubiri taarifa wakiwa Vatican walifurahia kuona moshi mweupe kutoka bomba la Kanisa la Sistine

Mchakato wa kumchagua papa waingia duru ya pili Mei 8

Makadinali 133 wa Kanisa Katoliki leo Mei 8, wanaingia katika duru ya pili ya upigaji kura wa papa mpya. Waumini wa Kanisa hilo duniani wanasubiri kwa hamu kuona moshi mweupe ambao ndio utaoashiria kupatikana kwa kiongozi mpya wa kanisa.
Mchakato huo, ulioanza Mei 7, ulitoa moshi mweusi, ukiwa na maana kwamba, bado papa mpya hajapatikana.

Mchakato wa kumchagua papa waingia duru ya pili Mei 8
Je, moshi mweupe kuonekana Mei 7, 2025?

Huku makadinali 133 wa Kanisa katoliki wakijifungia katika Kanisa la Sistine, Vatican kwa ajili ya kumchagua kiongozi mpya wa Kanisa hilo, waumini kote duniani wanangoja kuona ni lini moshi mweupe utaonekana katika jengo la kanisa hili kuashiria kupatikana kwa Papa mpya.

Vatican imesema Jumatano Mei 7, 2025, ishara ya moshi itatolewa mara moja lakini katika siku zijazo makadinali watapiga kura mara nne na hivyo moshi mweupe au mweusi kuonekana mara nne kwa siku.

Je, moshi mweupe kuonekana Mei 7, 2025?
Kwa nini uchaguzi wa papa hugubikwa na usiri?

Makadinali hufungiwa ndani ya kanisa na kunyang’anywa vifaa vyao vya mawasiliano ili kuwaepusha kufanya mawasiliano na ulimwengu wa nje ikiwemo waandishi wa habari.

Soma makala kamili
Kwa nini uchaguzi wa papa hugubikwa na usiri?
Makadinali na waumini wahudhuria misa takatifu

Makadinali na wafuasi wanahudhuria Misa Takatifu, kuadhimisha kuchaguliwa kwa papa mpya katika Kanisa la St. Peter, Basilica, Vatican, Mei 7, 2025.

Itakapofika saa kumi na moja jioni EAT, makadinali 133 watakaopiga kura watakusanyika katika Kanisa la Pauline Chapel na kufanya msafara hadi Sistine Chapel huku wakiimba.Wakifika Kanisa la Sistine, makadinali watakula kiapo cha usiri.

Baada ya hapo Mkuu wa Maadhimisho ya Kiliturujia ya Kipapa Diego Ravelli atatangaza “extra omnes” (“kila asiyepaswa kuwa hapa atoke nje”).Tamko hilo la “extra omnes” huashiria mwanzo wa mkutano.

Makadinali na waumini wahudhuria misa takatifu
Mchakato wa kumchagua Papa, kiongozi wa Kanisa Katoliki umeanza

Hakuna papa ambaye amechaguliwa katika siku ya kwanza ya kongamano kwa karne nyingi, kwa hivyo upigaji kura unaweza kuendelea kwa siku kadhaa.

Soma makala kamili
Mchakato wa kumchagua Papa, kiongozi wa Kanisa Katoliki umeanza
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us