SIASA
1 dk kusoma
Zaidi ya watu 100,000 wakimbia machafuko nchini DRC, Umoja wa Mataifa wasema
Machafuko yamekumba maeneo yenye utajiri wa madini nchini DRC, huku vikosi vya M23 vinavyoungwa mkono na Rwanda vikiendelea kudhibiti baadhi ya maeneo kadhaa mashariki mwa DRC.
Zaidi ya watu 100,000 wakimbia machafuko nchini DRC, Umoja wa Mataifa wasema
Machafuko yamekumba eneo lenye madini mengi la nchini DRC kwa miezi kadhaa sasa, huku vikosi vya M23 vinavyoungwa mkono na Rwanda vikiendelea kudhibiti baadhi ya maeneo Mashariki mwa DRC./Picha: Reuters
21 Machi 2025

Watu zaidi ya 100,000 wameyakimbia makazi yao nchini DRC ndani ya kipidi cha miezi mitano, Umoja wa Mataifa ulisema siku ya Ijumaa.

"Katika kipindi cha chini ya miezi mitatu, idaidi ya raia wa Congo wanaokimbilia nchi jirani imevuka 100,000," amesema msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR).

Machafuko yamekumba maeneo yenye utajiri wa madini nchini DRC, huku vikosi vya M23 vinavyoungwa mkono na Rwanda vikiendelea kudhibiti baadhi ya maeneo kadhaa mashariki mwa DRC.

Hatua hiyo imewalazimu majeshi ya serikali ya Congo kukimbia maeneo ya Kaskazini na Kusini mwa Kivu.

"Kulikuwa na wakimbizi wa ndani wapatao 400,000 katika eneo la Kivu Kaskazini, ," liliongeza shirika la UNHCR.

"Mashirika ya kibinadamu yanapata wakati mgumu kujenga makazi kutokana na masharti ya misaada kubadilika."

 

CHANZO:AFP
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us